• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watuishi |
Mlele District Council
Mlele District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya
    • Viengo
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Kilimo na Umwagiliaji
    • Huduma za Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orotha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Mazingira
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa
      • Kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayotekelezwa
    • Iliyotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma
    • Sheria Ndogo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kiini cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Album ya Picha
    • Video
    • Hotuba
  • TASAF

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homera

Posted on: March 5th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Juma Homera anaeleza fursa za Uwekezaji zilizopo katika Mkoa wa Katavi wakati wa Uzinduzi wa Mwongozo wa kitabu cha Uwekezaji Mkoani Katavi, Hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Mpanda Manispa Hall,  Machi 3’ 2021

Mkoa wa Katavi umezindua kitabu cha Mwongozo wa uwekezaji ili kutoa uelekeo wa uwekezaji kwa wawekezaji wa ndani ya nchi na nje Kitabu ambacho kitakuwa mwongozo wa kuwaongoza wawekezaji ambao wana karibishwa kuja kuwekeza.

Kuzinduliwa kwa kitabu hicho kutasaidia katika kuweka  mwelekeo mzuri wa kuonesha wapi wawekeze ambapo mkoa umeainisha maeneo ya uwekezaji katika sekta mbalimbali ziwe za kilimo,utalii,Biashara ujenzi wa viwanda.

Kuzinduliwa kwa kitabu hicho kutaleta mafanikio gani kwa jamii ya wanakatavi na Taifa kwa ujumla,zaidi ya miaka kumi iliyopita kuliwahi kufanyika kongamano la uwekezaji kwa Mikoa ya Ukanda Ziwa Tanganyika iliyojumuisha mikoa ya Kigoma, Katavi na Rukwa huku Mkoa wa Tabora ukikaribishwa kama mwalikwa.

Tangu kuwepo kwa kongamano hilo kumekuwepo mabadiliko mbalimbali,katika sekta za kiuchumi kiutamaduni na Nyanja nyingine za kijamii.

  Wawekezaji waliopata nafasi kushiriki katika Kongamano la  uzinduzi wa  Kitabu cha muongozo wa uwekezaji mkoani Katavi wamehimizwa kuchangamkia fursa za uwekezaji katika mkoa huo wenye zaidi ya hekta 45,000.

Akizungumza katika mkutano huo uliowakutanisha wadau wa uwekeaji kutoka maeneo mbalimbali, Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe Juma Homera ameeleza kuwa  katika ujenzi wa viwanda Mkoa umetenga hekari 245 kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda mbalimbali.

“Kutokana na wingi wa samaki wanaovuliwa kutoka ziwa Tanganyika wakiwemo, migebuka, kuhe, sangara pamoja na kamongo, Mkoa umetenga hekari 245 kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vya kusindika na kuchakata samaki” kwa mjibu wa Mkuu huyo wa Mkoa Mhe, Homera

Mkuu huyo wa Mkoa ameongeza kuwa wawekezaji wanayo fursa ya ujenzi wa viwanda mbalimbali vikiwemo viwanda vya usindikaji nafaka, ujenzi wa viwanda vya asali, uchakataji wa nyama na maziwa, pamoja na viwanda vya mbao.

Katika sekta ya utalii Mkuu wa Mkoa Homera amesema wawekezaji wanayofursa ya kuwekeza, kwa upande wa makampuni ya utalii yatakayosaidia ongezeko la utalii katika Mkoa huo, wenye vivutio vingi vva utalii ikiwemo mto mapacha wenye maji yanayosadikika kuwa ukiyanywa maji hayo unazaa watoto mapacha,eneo la chemichemi ya maji  moto pamoja na hifadhi ya Taifa Katavi yenye ukubwa wa hekari 4471 na ambayo inawanyama wakubwa kuliko maeneo mengine hapa nchini.

Mhe, Homera anasema kuwa hapa nanukuu “Tuna zaidi ya sokwe 2500, tuna twiga mweupe ambaye huwezi kumpata kokote Tanzania isipokuwa Mkoani katavi, lakini pia tunao Viboko na Tembo wakubwa sana kama nyumba” Anasema Mhe, Homera.

Mapema Prof Leonard Mwaikambo ambaye alihusika katika kuandaa na  kuandaa andiko kitabu cha   Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Katavi ameeleza taasisi ya kiuchumi ya kijamii wamekuwa wakibainisha  vivutio vya uwekezaji.

Mpaka sasa  Mikoa 17 imezindua mwongozo ukiwamo Mkoa wa Katavi,fursa kubwa za kilimo ufugaji na utalii,fursa zikitumika vizuri zitaboresha maisha ya wanajamii ya Mkoa wa Katavi na watanzania kwa ujumla.

  Akizungumza katika Kongamano la uzinduzi wa Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji kwa niaba ya Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Uwekezaji Prof, Kitila Mkumbo ameleza kufurahishwa na juhudi za Mkoa katika kuvutia wawekezaji kwa kuandaa mipango yao mizuri inayowavutia wawekezaji.

 Prof Mkumbo amesema Mkoa wa Katavi ni muhimu kwa nchi yetu kwenye kilimo,madini na utalii na wana äkili ya uwekezaji.

Amesema Mfumo wa kiuchumi wa fedha duniani unahitaji watu wenye uwezo wa kufanya kazi kwa bidii, mwekezaji ni lazima awe na pesa nyingi.

Wawekezaji wapo wa aina mbalimbali wa ndani na wa nje  Serikali na wadau mbalimbali,kwa mantiki hiyo watumishi watambue kuwa wajibu wao ni  kutengeneza mazingira mazuri ya wawekezaji.

Amesema wawekezaji wakifanikiwa ndipo serikali nayo inapopata mapato,katika kukuza uchumi nchi inahitaji wawekezaji.

Kwa mtumishi wa Serikali yeyote anayekwamisha wawekezaji anakwamisha mipango ya Serikali, Serikali na Serikli haitamuonea aibu itaßhughulika naye, na itawalinda  wawekezaji ambao ni wazuri,.

   Prof Mkumbo amesema ni jukumu la Mkoa kuwawesha wawekezaji na kazi ya wizara ikishirikiana na mikoa katika kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji.

Mwongozo wa Serikali hawataki kuona wawekezaji  wananyanyaswa,wawekezaji watimize wajibu wao kwa kufuata

sheria za nchi,ingawa wapo wachache wenye changamoto watapambanao kwa kufuata sharia.

Amemalizia kwa kueleza kuwa serikali inataka kuweka mwongozo namna wanavyoweza kuwekeza katika kuwakodisha na kuwahudumia na




Matangazo

  • TANGAZO KUITWA KWENYE USAILI March 15, 2021
  • WIMBO WA MWENGE April 09, 2017
  • TANGAZO LA KUNYWA DAWA ZA MINYOO YA TUMBO April 26, 2017
  • Nafasi za kazi mbalimbali serikalini July 11, 2018
  • Waonaji wote

Habari Mpya

  • picha ya waumini kanisani

    March 25, 2021
  • Ibada maalum ya Maombolezo.

    March 25, 2021
  • Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uwekezaji) Prof. Kitila Mkumbo

    March 05, 2021
  • Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homera

    March 05, 2021
  • Waonaji wote

Video

KATUNI SAFI KWA AJILI YA WATOTO
Video Zaidi

wavuti za Haraka

  • FACE BOOK PAGE YA MLELE
  • MLELE DC BLOG
  • kilimo na umwagiliaji
  • mafunzo tovuti za serikali kanda ya magharibi
  • MAONESHO

Wavuti Mwambata

  • Wizara ya Utumishi wa Umma
  • Tume ya ajira ya Tanzania
  • Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania
  • Jamhuri ya muungano wa tanzania
  • Tawala za mikoa na Serikali za mitaa
  • BARAZA LA MITIHANI

Takwimu za Watembeleaji

world map hits counter

Hesabu Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mlele

    Anuani ya Posta: S.L.P 686 MPANDA

    Simu: +255759023788

    Simu ya Kiganjani: 0759023788

    Barua pepe: ded@mleledc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ya @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Mlele. Hakizote zimehifadhiwa