• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watuishi |
Mlele District Council
Mlele District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Maji
        • Historia
        • Dhima na Dira
        • Muundo wa Taasisi
        • Ukaribisho
        • Jaribu
        • what we do
        • Huduma ya Maji
        • Huduma za Afya
        • Elimu Msingi
        • Huduma
        • Mwenyekiti wa Halmashauri
        • Mkurugenzi Mtendaji
        • Utawala na Rasilimali watu
        • /TEHAMA-na-Takwimu
        • Idara ya Afya na Ustawi wa Jamii
        • Mipango takwimu na Ufuatiaji
        • Ardhi na Maliasili
        • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Sheria
        • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maendeleo ya Jamii
        • Idara
        • Vitengo
        • Ujenzi
        • Maji
        • Ugavi na Manunuzi
        • Usafishaji na Mazingira
        • Uchaguzi
        • Tasaf III
        • Mainstreaming Sustainable Forest Managment in Woodland of Western Tanzania Project
        • Mwenge waUhuru
        • UKIMWI/ VVU
        • Risk Oficer Cordinator
        • Miradi inayoendelea
        • Zabuni
        • Kazi za Idara Utumishi
        • Muundo wa Halmashauri
        • Miradi Lengwa
        • Kitengo cha nyuki
        • Mwenge
        • Sera ya Faragha
        • Kanusho
        • Machapisho
        • Sheria
        • MTF
        • Fomu
        • Orodha ya Madiwani
        • Fedha, Uongozi na Mipango
        • UKIMWI
        • Maji
        • Mipango Miji na Mazingira
        • Uchumi, Afya na Elimu
        • Maadili
        • Ratiba
        • Vikao vya waheshimiwa
        • Kuonana na Mwenyekiti
        • Madiwani
        • Kanausho
        • Huduma ya Maji
        • Huduma ya Afya
        • Huduma ya Kilimo
        • Huduma ya Elimu
        • Huduma ya Ufugaji
        • Huduma za Uvuvi
        • Huduma za Sheria
        • Huduma za kiutumishi
        • Vivutio vya Utalii
        • Kilimo
        • Ufugaji
        • Itakayo tekelezwa
        • Inayoendelea
        • Iliyo Tekelezwa
        • muongozo
        • Sheria Ndogo
        • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
        • Mpango Mkakati
        • Taarifa
        • Fomu Mbalimbali
        • Taarifa kwa Umma
        • Video za shughuli zetu
        • Maktaba ya Picha
        • Magazeti
        • Hotuba
        • ORODHA YA WAJUMBE WA KAMATI MBALIMBALI ZA KUDUMUKWA MWAKA WA FEDHA 2019/2020
        • KARENDA YA VIKAO VYA KISHERIA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA MLELE KWA MWAKA WA FEDHA 2019/2020
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya
    • Viengo
      • Kitengo cha TEHAMA na Mahusiano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Uchaguzi Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Kilimo na Umwagiliaji
    • Huduma za Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orotha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Mazingira
      • UKIMWI
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa
      • Kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayotekelezwa
    • Iliyotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kiini cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Album ya Picha
    • Video
    • Hotuba
  • TASAF

MAPATO YAONGEZEKA NA KUTOA SURA MPYA TANZANIA

Posted on: October 7th, 2018

Serikali imesema kuwa  mwaka wa fedha 2017/2018 jumla ya Sh bilioni 553.39 zimekusanywa kati ya Sh bilioni 687.31 ambazo ni sawa na asilimia 81 ya lengo ambalo halmashauri zote nchini ilijiwekea.

Aidha, Dodoma imeongoza katika ukusanyaji wa mapato kwa upande wa majiji na mikoa ambapo Halmashauri ya Mji Geita ikiwa kinara katika mlinganisho wa kiasilimia kwa Mamlaka zote za Serikali za Mitaa bila ya kujali hadhi huku halmashauri ya Mbinga ikishika mkia.

Akitangaza makusanyo kwa halmashauri zilizofanya vizuri na vibaya, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo alisema: " TAMISEMI imekuwa ikifuatilia ukusanyaji wa mapato katika halmashauri zake ili kuweza kufanikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika halmashauri zote nchini.

" Baada ya kumaliza zoezi la usuluhishi wa kibenki takwimu zinaonyesha kwamba kwa mwaka wa fedha 2017/2018 jumla ya shilingi 553,390,075,912 zimekusanywa kati ya shilingi 687,306,661,000 ambazo ni sawa na asilimia 81 ya lengo."

Jafo alisema kwa upande wa Majiji, Jiji la Dodoma limekuwa la kwanza kati ya majiji sita likiwa limekusanya Sh bilioni 25.06 kati ya Sh bilioni 19.33 ambayo ni sawa na asilimia 130 ya lengo wakati Jiji la Mbeya limekuwa la mwisho kwa kukusanya kiasi cha Sh bilioni 7.82 kati ya Sh bilioni 11.0, sawa na asilimia 71.

Dar es Salaam ni ya pili ikiwa imekusanya Sh bilioni 15.67 kati ya makisio ya Sh bilioni 16.41 ambayo ni asilimia 95, Arusha ya tatu ikikusanya Sh bilioni 13.59 kati ya lengo la Sh bilioni 14.58, Mwanza imeshika nafasi ya nne ikikusanya Sh bilioni 10.47 kati ya malengo ya Sh bilioni 1.44, Tanga ikikusanya Sh bilioni 10.84 kati ya malengo ya Sh bilioni 14.03.

Jafo alisema Manispaa ya Iringa ndiyo ilikuwa ya kwanza kwa kukusanya Sh bilioni 4.28  kati ya Sh 4.17 ambayo sawa na asilimia 103 ikifuatiwa na Manispaa ya Temeke iliyokusanya Sh bilioni 29.41 kati ya lengo la kukusanya Sh bilioni 29.07 sawa na asilimia 101.

Alisema katika kundi hili, Manispaa ya Ilemela ilikuwa ya mwisho kwa kukusanya Sh bilioni 4.76  kati ya lengo la kukusanya Sh bilioni 11.75 sawa na asilimia 40.

Jafo alisema Halmashauri ya Mji wa Geita ndiyo ilikuwa ya kwanza kwa kukusanya Sh bilioni 6.86 kati ya lengo la kukusanya Sh bilioni 3.15 sawa na asilimia 218 ikifuatiwa na Halmashauri ya Mji wa Njombe iliyokusanya Sh bilioni  2.93 kati ya lengo la kukusanya Sh bilioni 2.40 sawa na asilimia 122.

Alisema Halmashauri ya Mji wa Nanyamba ni ya mwisho kwa kukusanya Sh bilioni 1.14 kati ya lengo la kukusanya Sh bilioni 2.11 sawa na asilimia 54.

Jafo alisema Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ilikuwa kinara kwa kukusanya Sh bilioni 3.09 kati ya Sh bilioni 1.87 sawa na asilimia 165 ikifuatiwa na Halmashauri ya Mpimbwe iliyokusanya Sh bilioni 1. 55 kati ya Sh milioni 956.84 sawa na asilimia 162.

Alisema halmashauri za wilaya zilizofanya vibaya zaidi ni pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga iliyokusanya asilimia 20, halmashauri ya Songea iliyokusanya asilimia 33, Halmashauri ya Rorya ilikusanya asilimia 37 na Halmashauri ya Siha iliyokusanya asilimia 39.

Aidha, Jafo alisema katika mlinganisho wa kiasilimia kwa Mamlaka zote za Serikali za Mitaa bila ya kujali hadhi zao, halmashauri tatu kinara kwa makusanyo kiasilimia ni Halmashauri ya Mji wa Geita ambayo imekusanya kwa asilimia 218, Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ambayo imekusanya kwa asilimia 165 na Halmashauri ya Mpimbwe iliyokusanya kwa asilimia 162 .

" Vivyo hivyo, Hamashauri tatu ambazo zimekusanya kwa asilimia ndogo zaidi ni pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga iliyokusanya kwa asilimia 20, Halmashauri ya Wilaya ya Songea asilimia 33 na Halmashauri ya Wilaya ya Rorya iliyokusanya kwa asilimia 37."

Jafo alisema kwa mwaka wa fedha 2017/2018,  halmashauri 38 sawa na asilimia 24 ya Halmashauri zote nchini ziliweza kuvuka malengo yake ya mwaka ambazo ni  Geita TC, Kibaha DC, Mpimbwe DC, Kaliua DC, Misungwi DC, Bukoba DC, Pangani DC, Kilindi DC, Kilombero DC, Kibondo DC, Makete DC, Dodoma CC, Wanging'ombe DC, Longido DC, Ulanga DC, Kasulu DC, Bukombe, Njombe TC, Ushetu DC, Handeni TC, Mpanda DC, Muleba DC, Babati DC, Mwanga DC, Kibaha TC, Bunda TC, Mbozi DC, Ukerewe DC, Tandahimba DC, Magu DC, Newala DC, Monduli, Malinyi DC, Lushoto DC, Njombe DC, Iringa MC, Tarime DC, na Temeke MC

Pia halmashauri 14 sawa na asilimia 7.57 hazikuweza kufikia asilimia 50 ya malengo yake ambazo ni  Iringa DC, Kyerwa DC, Mbulu DC, Kishapu DC, Igunga DC, Chato DC, Itilima DC, Itigi DC, Ubungo MC, Ilemela MC, Siha DC, Rorya DC, Songea  DC, na Mbinga DC

Jafo alisema mamlaka nne ziliibuka kinara kwa kukusanya mapato mengi ambazo ni Manispaa ya Ilala (Sh bilioni 44.51), Kinondoni (Sh bilioni 29.75), Temeke (Sh bilioni 29.41) na Dodoma ilikusanya Sh bilioni 25.06.

Alisema pia halmashauri tatu zilizokusanya mapato kidogo bila kujalisha asilimia ya makusanyo yao ni pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko (Sh milioni 347.15), Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe (Sh milioni 37.22) na Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma (Sh milioni 418.79).

Jafo alisema halmashauri za mikoa mitatu ziliifanya Mikoa yao kuwa kinara kwa makusanyo ya mapato ya ndani ambayo imeongozwa na Dodoma iliyokusanya kwa asilimia 170, Geita imekusanya kwa asilimia 104 na Njombe uliokusanya kwa asilimia 103.

" Mikoa hii mitatu ndiyo iliyovuka malengo yake katika ukusanyaji wa mapato kwa mwaka uliopita.".

Jafo alisema mikoa mitatu ambayo ilikusanya kwa asilimia ndogo ni pamoja na Ruvuma uliokusanya kwa asilimia 46, Simiyu asilimia 59 na Shinyanga asilimia 66.

Akizungumzia mikakati ya uamarishaji wa makusanyo kwa mwaka wa fedha 2018/2019, Jafo aliziagiza halmashauri zote zilizokusanya chini ya asilimia 50 ya lengo kwa mwaka uliopita zimetakiwa  kutoa maelezo ni kwanini hazikufikia hata asilimia 50 ya lengo walilojiwekea.

" Nawaelekeza Wakuu wa Mikoa kufuatilia ufujaji wa mapato katika Halmashauri zilizopo kwenye Mikoa yenu ili kubaini wanaohusika kufanya uzembe wa aina yoyote uliojitokeza katika ukusanyaji wa mapato kwenye Halmashauri hizo ili endapo itabainika kulikuwa na hujuma ya makusudi kwenye ukusanyaji chukueni hatua za kinidhamu na kisheria.

Aliongeza: " kwasababu wastani wa makusanyo ni asilimia 81, basi hii itakuwa ndio kiwango chetu cha chini, hivyo kwa mwaka wa fedha 2018/2019 ni kila Halmashauri katika Mikoa yote isikusanye chini ya asilimia 81 ya lengo lake.  Hivyo, Wakuu wa Mikoa mnapaswa kusimamia mkakati huu katika Mikoa yenu.

Pia Jafo aliwataka wakuu wa mikoa kusimamia halmashauri zao ili kudhibiti matumizi ya mapato ya ndani yanayokusanywa kwa lengo la kufanikisha Miradi ya maendeleo kwa wananchi.

Aidha, Jafo alisema wakurugenzi watapimwa utendaji wao kwa kuangalia suala la utekelezaji wa mapato kwa mwaka 2018/19.

" Kwa mwaka 2018/2019, pia tutaangalia suala la makusanyo na matumizi, maana kukusanya ni jambo jingine na kutumia ni jambo jingine, hivyo tuanaangalia katika kilichokusanywa ni kiasi gani kimepelekwa kutekeleza miradi ya maendeleo."

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Tamisemi, Mhandisi Mussa Iyombe alisema pamoja na kufuatilia kwa karibu halmashauri ambazo zimefanya vibaya katika ukusanyaji mapato, lakini pia itaziangalia zile ambazo zingeweza kukusanya maradufu ya lengo ili kuangalia kama ziliweka makisio ya chini ili baadae zionekane zinafanya vizuri.

" Katika hili hatutamuonea mtu, na hata hatutamfumbia macho mtu yeyote ambaye ameshindwa kuwajibika katika nafasi yake, lakini tutaziangalia hata zile halmashauri ambazo uchumi wake ni mzuri lakini kwenye makusanyo hazikufanya vizuri sambamba na zile ambazo zimeweka makisio ya chini," alisema.

Matangazo

  • TANGAZO KUTOKA TUME HURU YA UCHAGUZI March 03, 2025
  • MABADILIKO YA UKUMBI WA USAILI MLELE DC October 04, 2024
  • Tangazo la Ajira ya ukusanyaji wa Mapato July 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI MBALIMBALI ZA AFYA December 10, 2021
  • Waonaji wote

Habari Mpya

  • MIRADI YA MWENGE 2025

    July 01, 2025
  • SIKU YA WAJANE DUNIANI

    June 23, 2025
  • ZIARA YA MAFUNZO MANISPAA YA MOSHI {UKUSANYAJI WA MAPATO}

    June 19, 2025
  • ZIARA YA MAFUNZO MANISPAA YA MOSHI {UDHIBITI WA TAKA NGUMU}

    June 20, 2025
  • Waonaji wote

Video

#TBC LIVE ZOOM: YALIYOJIRI NA MAFANIKIO YA ZIARA YA RAIS SAMIA NCHINI QATAR
Video Zaidi

wavuti za Haraka

  • FACE BOOK PAGE YA MLELE
  • MLELE DC BLOG
  • kilimo na umwagiliaji
  • mafunzo tovuti za serikali kanda ya magharibi
  • MAONESHO
  • Tuma barua pepe hapa

Wavuti Mwambata

  • Wizara ya Utumishi wa Umma
  • Tume ya ajira ya Tanzania
  • Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania
  • Jamhuri ya muungano wa tanzania
  • Tawala za mikoa na Serikali za mitaa
  • BARAZA LA MITIHANI

Takwimu za Watembeleaji

world map hits counter

Hesabu Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mlele

    Anuani ya Posta: S.L.P 686 MPANDA

    Simu: +25525295197

    Simu ya Kiganjani: 0786077372

    Barua pepe: ded@mleledc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ya @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Mlele. Hakizote zimehifadhiwa