• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watuishi |
Mlele District Council
Mlele District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Maji
        • Historia
        • Dhima na Dira
        • Muundo wa Taasisi
        • Ukaribisho
        • Jaribu
        • what we do
        • Huduma ya Maji
        • Huduma za Afya
        • Elimu Msingi
        • Huduma
        • Mwenyekiti wa Halmashauri
        • Mkurugenzi Mtendaji
        • Utawala na Rasilimali watu
        • /TEHAMA-na-Takwimu
        • Idara ya Afya na Ustawi wa Jamii
        • Mipango takwimu na Ufuatiaji
        • Ardhi na Maliasili
        • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Sheria
        • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maendeleo ya Jamii
        • Idara
        • Vitengo
        • Ujenzi
        • Maji
        • Ugavi na Manunuzi
        • Usafishaji na Mazingira
        • Uchaguzi
        • Tasaf III
        • Mainstreaming Sustainable Forest Managment in Woodland of Western Tanzania Project
        • Mwenge waUhuru
        • UKIMWI/ VVU
        • Risk Oficer Cordinator
        • Miradi inayoendelea
        • Zabuni
        • Kazi za Idara Utumishi
        • Muundo wa Halmashauri
        • Miradi Lengwa
        • Kitengo cha nyuki
        • Mwenge
        • Sera ya Faragha
        • Kanusho
        • Machapisho
        • Sheria
        • MTF
        • Fomu
        • Orodha ya Madiwani
        • Fedha, Uongozi na Mipango
        • UKIMWI
        • Maji
        • Mipango Miji na Mazingira
        • Uchumi, Afya na Elimu
        • Maadili
        • Ratiba
        • Vikao vya waheshimiwa
        • Kuonana na Mwenyekiti
        • Madiwani
        • Kanausho
        • Huduma ya Maji
        • Huduma ya Afya
        • Huduma ya Kilimo
        • Huduma ya Elimu
        • Huduma ya Ufugaji
        • Huduma za Uvuvi
        • Huduma za Sheria
        • Huduma za kiutumishi
        • Vivutio vya Utalii
        • Kilimo
        • Ufugaji
        • Itakayo tekelezwa
        • Inayoendelea
        • Iliyo Tekelezwa
        • muongozo
        • Sheria Ndogo
        • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
        • Mpango Mkakati
        • Taarifa
        • Fomu Mbalimbali
        • Taarifa kwa Umma
        • Video za shughuli zetu
        • Maktaba ya Picha
        • Magazeti
        • Hotuba
        • ORODHA YA WAJUMBE WA KAMATI MBALIMBALI ZA KUDUMUKWA MWAKA WA FEDHA 2019/2020
        • KARENDA YA VIKAO VYA KISHERIA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA MLELE KWA MWAKA WA FEDHA 2019/2020
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya
    • Viengo
      • Kitengo cha TEHAMA na Mahusiano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Uchaguzi Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Kilimo na Umwagiliaji
    • Huduma za Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orotha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Mazingira
      • UKIMWI
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa
      • Kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayotekelezwa
    • Iliyotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kiini cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Album ya Picha
    • Video
    • Hotuba
  • TASAF

miradi ya Maendeleo

Posted on: January 12th, 2021

 

                               HALMASHAURI YA WILAYA YA MLELE





                      

                                                                                                                  S.L.P 686,

Simu:

Nukushi:

E-mail: ded@mleledc.go.tz

Barua@mleledc,go.tz                                                                   MLELE –KATAVI.

                                                                                                         16/12/2020.

 

Tovuti: www.mleledc.go.tz  

TAARIFA KWA UMMA.                                                                                                                                         

YALIYOJIRI KATIKA MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA MLELE TAREHE 16 DISEMBA 2020.

Mwenyekiti mpya wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Mheshimiwa Soud Mlolwa Mbogo leo tarehe 16 Disemba amefunga Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mlele.

Mheshimiwa Mbogo amefunga Mkutano huo wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mlele ikiwa ni  mara ya kwanza baada ya kuchaguliwa na Madiwani kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele.

Katika hotuba yake ya ufunguzi Mheshimiwa Mbogo ametoa shukurani zake kwa Chama cha Mapinduzi CCM, wananchi pamoja na Madiwani wa  Halmashauri ya Wilaya ya Mlele kwa kumwamini na kumpa ridhaa ya kuliongoza Baraza la Madiwani kwa kipindi cha miaka mitano.

Katika Mkutano huo wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Waheshimiwa Madiwani wamekula kiapo cha uadilifu kwa wote na kuahidi  kuwa wazalendo,  pia kuahidi kufanya kazi  kwa kutanguliza mbele masilahi mapana ya Taifa  kwa kuwatumikia wananchi wa Halmashauriya Wilaya ya Mlele. 

Mheshimiwa Mbogo ametoa wito kwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele kutimiza wajibu wao mkubwa waliopewa na wananchi kwa kuhakikisha kuwa wanafanya kazi kwa bidii,uweledi na maarifa ili kuwaletea wananchi Maendeleo kwa  kuwa uchaguzi umekwisha kilichobakia ni kuchapa kazi  na kuwaletea wananchi maendeleo.

Aidha amewataka Madiwani wa Halmashauri ya Mlele kushirikiana vema na wataalam kuhakikisha wanatimiza majukumu yao ipasavyo  kusimamia ukusanyaji wa mapato,Suala la kilimo,Elimu Afya na Miundombinu mingine ili kuwaletea wananchi maendeleo.

  Mheshimiwa Mbogo amewaeleza Madiwani na Watalaam wa Halmashauri ya wilaya ya  Mlele kuwa wanalo jukumu kubwa la kuhakikisha kuwa wanatumia rasilimali zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele ikiwemo ardhi, mistu mifugo na kila aina ya rasilimali na kusimamia ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ili kufikia malengo mahususi ya kuwaletea wananchi Maendeleo.  

Amesisitiza Ofisi ya Mkurugenzi kushughulikia changamoto mbalimbali zilizopo ikiwa ni pamoja na kusimamia mikutano ya ngazi ya   Vijiji  na Kata inafanyika,  pamoja na kuhamasisha uzalishaji wa mazao ya kimkakati yanalimwa ambayo ni zao la Pamba ,Korosho na Ufuta ili kuhakikisha kuwa mazao hayo yanabadilisha hali ya mapato ya Halmashauri.

Mapema Katibu tawala wa Wilaya ya Mlele LIinkolin Tamba akifungua Mkutano huowa Madiwani amesisitiza ushirikiano wa karibu kati ya wataalam na Waheshimiwa Madiwani ili kuwaletea wananchi maendeleo.

Akawataka ametoa rai kwa  Waheshimiwa hao kuchapa kazi na kusimamia sera za serikali ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Zahanati kwa kila Kijiji ,Ujenzi wa Vituo vya Afya kila kata kwa zile Kata ambazo hazijakamilisha wahakikishe wana kamilisha,ikiwa ni pamoja na kuhakiksha watoto wote waliofaulu mtihani wa Darasa la saba wabakwenda shule sanjali na kukamilisha utengenezaji wa madawati kwa ajili ya wananfunzi wa shule za Sekondari .

Aidha amepongeza kwa Halmashauri kufanya vizuri katiaka matoke ya mtihani wa Darasa la Saba ambapo Kimkoa imekuwa ya kwanza, na Kikanda pia imefanya vizuri hadi kuwa ndani ya kumi bora kitaifa. Juhudi hizo ni za kupongezwa.

Katika Mkutano huo wa Baraza la Madiwani pia Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Mwalimu Alexus Revocatus Kagunze  amewasilisha Taarifa ya utekelezaji wa Kazi zilizofanyika kipindi Waheshimiwa Madiwani hawapo,taarifa iliyoeleza mafanikio mbalibmbali na mikakati ya kimaendeleo ya Halmashauri haya katika upande wa ukusanyaji wa Mapato,hali iliyoonesha wamefanya vizuri katika katika kusimamia maendeleo.

Baada ya Taarifa hiyo waheshimiwa madiwani waliipokea na kujadili kasha wakapongeza kwa kazi nzuri iliyofanyika kipindi hawapo madarakani baraza lilipovunjwa.

Mkutano ambapo umeshuhudia kuundwa kwa kamati za kudumu na kuchaguliwa wenyeviti wake umeahirishwa hadi hapo utakapoitishwa tina kwa mjibu wa kanuni taratibu na sheria.

Imetolewa na

 Kibada Ernest  Msafiri.

Afisa Habari na Mahusiano.

HALMASHAURI YA WILAYA YA MLELE





                      

                                                                                                                  S.L.P 686,

Simu:

Nukushi:

E-mail: ded@mleledc.go.tz

Barua@mleledc,go.tz                                                                   MLELE –KATAVI.

                                                                                                         06/01/2020.

 

Tovuti: www.mleledc.go.tz 

TAARIFA KWA UMMA.

YALIYOJIRI WAKATI WA ZIARA YA MKUU WA MKOA WA KATAVI HALMASHAURI YA WILAYA YA MLELE TAREHE 05 JANUARI  2020.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe, Juma Homera akiwa ameambatana na Viongozi mbalimbali wa Mkoa katika Halmashauri ya wilaya ya Mlele alitembelea Ujenzi wa Jengo  la Utawala,Halmasahuri ya Wilaya ya Mlele,Ujenzi wa Kituo cha Afya inyonga B,Ujenzi wa Hospitali ya wilaya,Ujenzi wa Kiwanda cha kuchakata  asali,na Ujenzi wa kituo cha kupokelea umeme wa gridi ya Taifa kilichoko kijiji cha Utende lengo la ziaa hiyo ilikuwa kuhamasisha na kusisitiza  usimamiaji wa miradi hiyo hasa majengo ya Serikali yanajengwa kwa ubora na gharama nafuu.

Akizungumza na watendaji na watalaam wa Wilaya ya Mlele amesema  ni vyema wakahakikisha kuwa wanasimamima miradi hiyo ya serikali kwa uadilifu na ujenzi uwe wa gharama nafuu.

Mkuu wa Mkoa Juma Homera  katika ziara yake alifanya mikutano ya Hadhara kuzungumza na wananchi wa Kijiji cha Kamalampaka na Kamsisi  wakati wa Ziara yake aliyoifanya na kutoa maelekezo.

-Alifurahishwa na kiwango cha ufaulu wa wanafunzi shule za Msingi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele kwa kuwa miongoni wa Shule kumi bora Kitaifa na kikanda na kushika nafasi ya kwa kwanza kimkoa katika ufaulu alitoa pongeza Kwa Halmshauri ya Mlele kwa kufanya vizuri.

Kuhusu watoto waliofaulu ametoa maelekezo yafuatayo  ili kuhaikikisha wote waliofaulu wanaendelea  na masomo ya Sekondari,na wale ambao hawakupata nafsai ya kuendelea na masomo ya  Sekondari wapelekwe chuo cha maendeleo ya jamii Msaginya na chuo cha Ufundi stadi VETA Mpanda.

-Amewataka walimu wa shule za Msingi na Sekondari kuw an utaratibu utakaonesha namna ya kuwabaini wanafunzi ambao hawajaripoti na kuwafuatilia na wawe na kumbukumbu na kuwathamini wanafunzi na walimu wanaofanya vizuri na kuwapa motisha. 

-Halmashauri kusimamia zoezi la utengenezaji madawati ili kuhakikisha utengenezaji wa madawati unakamilika na watoto waliofaulu kwenda kidato cha kwanza sekondari wanaripoti pindi shule zitakapofunguliwa na asiwepo mtoto wa kukaa chini,Halmashauri inaupungufu wa dawati karibu 700.

-Kuhakikisha wazazi wote wanawapeleka shule watoto pindi shule zitakapofunguliwa na asiwepo motto wa kushindwa kwenda shule kwa kisingizio cha kukosa ada kwa kuwa elimu sasa ni bure.

-Ugawaji wa mashamba ufanyike ndani ya siku 14 tangu kutolewa kwa maelekezo yake,kwa wale walionunua mashamba katika eneo ambalo lilikuwa na mfutano na wakala w a huduma za mistu TFS mgogoro huu umepatiwa ufumbuzi na watu wagawiwe wale walionunua na ugawaji ufute utaratibu kila mtu apate angalau kidogo kwa kuwa orodha ipo, na wao fedha zilizotumika kununulia maeneo hayo zilitumika kujenga Zahanati ya Kijiji cha Kamsisi.

Waheshimiwa Madiwani wasimamie ipasavyo miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri kwenye maeneo yao  na iendani na thamani ya fedha ya Serikali.

Amesisitiza suala la amani,utulivu na mshikamano kwa kueleza kuwa Mkoa wa Katavi uko salama.

-Amewakumbusha wakulima kujikita katika mazao ya  Korosho,ufuta,na alzeti  karanga ,bila kusahau mazao ya chakula mahindi,na mpunga, akizungumzia kuhusu zao la pamba amesema walime kwa wingi kwa  kuwa soko lipo, na tayari kiwanda  cha kuchambua pamba kipo Mkoani hapa kimejengwa katika Wilaya ya TANGANYIKA hivyo skuhusu soko kwa sssa hakuna wasiwasi pamba yote itakayolimwa katika mkoa wa Katavi na maeneo mengine itanunuliwa.,

Imetolewa na

 Kibada Ernest  Msafiri.

                                                                                                                                                                                                                    Afisa Habari na Mahusiano

                                                                                                                                                                                                               Halmashauri ya wilaya ya Mlele.

Matangazo

  • TANGAZO KUTOKA TUME HURU YA UCHAGUZI March 03, 2025
  • MABADILIKO YA UKUMBI WA USAILI MLELE DC October 04, 2024
  • Tangazo la Ajira ya ukusanyaji wa Mapato July 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI MBALIMBALI ZA AFYA December 10, 2021
  • Waonaji wote

Habari Mpya

  • MAENDELEO YA UJENZI WA SHULE SHIKIZI

    April 03, 2025
  • KIKAO CHA WAMILIKI WA VIWANDA VYA KUCHAKATA UNGA

    March 14, 2025
  • MAMLAKA YA ELIMU TANZANIA TEA KUKABIDHI MIRADI

    February 22, 2025
  • MSAADA WA MADAWATI 136

    January 30, 2025
  • Waonaji wote

Video

#TBC LIVE ZOOM: YALIYOJIRI NA MAFANIKIO YA ZIARA YA RAIS SAMIA NCHINI QATAR
Video Zaidi

wavuti za Haraka

  • FACE BOOK PAGE YA MLELE
  • MLELE DC BLOG
  • kilimo na umwagiliaji
  • mafunzo tovuti za serikali kanda ya magharibi
  • MAONESHO
  • Tuma barua pepe hapa

Wavuti Mwambata

  • Wizara ya Utumishi wa Umma
  • Tume ya ajira ya Tanzania
  • Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania
  • Jamhuri ya muungano wa tanzania
  • Tawala za mikoa na Serikali za mitaa
  • BARAZA LA MITIHANI

Takwimu za Watembeleaji

world map hits counter

Hesabu Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mlele

    Anuani ya Posta: S.L.P 686 MPANDA

    Simu: +25525295197

    Simu ya Kiganjani: 0786077372

    Barua pepe: ded@mleledc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ya @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Mlele. Hakizote zimehifadhiwa