• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watuishi |
Mlele District Council
Mlele District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya
    • Viengo
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Kilimo na Umwagiliaji
    • Huduma za Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orotha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Mazingira
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa
      • Kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayotekelezwa
    • Iliyotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma
    • Sheria Ndogo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kiini cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Album ya Picha
    • Video
    • Hotuba
  • TASAF

Huduma ya Maji

TAARIFA YA UTEKELEZAJI - IDARA YA MAJI KWA KIPINDI CHA MWEZI JULAI HADI DISEMBA KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017

UTANGULIZI 

Idara ya maji ni miongoni mwa Idara zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele.  Katika kutekeleza shughuli zake, imegawanyika katika vitengo vifuatavyo:-

  1. Uendeshaji na Matengenezo (rehabilitation)
  2. Ujenzi na usimamizi wa miradi mipya ya maji (construction),

Halmashauri ilikuwa na jumla ya wananchi 34,960 kwa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012, kwa mwaka 2016 Halmashauri yetu inakadiriwa kuwa na wananchi 39,654 ikiwa ni wastani wa ongezeko la watu kwa asilimia 3.2 kila mwaka. Mpaka sasa ni asilimia 42.1 ya wananchi ndio wanaopata huduma ya maji safi na salama. 

Watumishi wa Idara

Idara hii ina jumla ya watumishi 5 katika mchanganuo ufuatao:-

  1. Mhandisi wa maji Mmoja (1)
  2. Mhandisi ujenzi mmoja (1)
  3. Fundi sanifu - ujenzi mmoja (1)

Fundi sanifu - maji (2, Mmoja kujitolea)

 

HALI YA USAMBAZAJI HUDUMA YA MAJI 

Hali ya usambazaji wa huduma ya Maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele inategemea uwepo wa miundo ifuatayo:-

Visima virefu

Halmashauri ya wilaya ya Mlele ina visima virefu 134 ambavyo vinatumia pampu ya mkono katika kutoa huduma ya maji kwa wananchi.

Visima vifupi

Halmashauri ya wilaya ya Mlele haina visima vifupi

Miradi ya maji ya kusukuma kwa mashine inayotumia dizeli

Katika kuhakikisha upatikanaji wa maji kwa wananchi Halmashauri ya Wilaya ya Mlele itatekeleza ujenzi wa miradi ya kusukuma kwa mashine inayotumia dizeli/umeme jua kwa ajili ya kuwapatia wananchi huduma ya maji. 

Miradi ya maji safi na usafi wa mazingira itakayotekelezwa ni miradi ya maji katika vijiji vya Nsenkwa, Mapili, Ilunde, Wachawaseme, Inyonga na Kamsisi.

Miradi tajwa hapo juu ipo hatua ya zabuni na utekelezaji wake utaanza Januari, 2017.

Miradi iliyokamilika ni ukarabati wa visima, uchimbaji wa visima ishirini na moja katika vijiji vya Kamsisi, Songambele, Imalauduki, Inyonga, Kalovya, Kamalampaka, Mapili, Ipwaga, Mlogoro, Kaulolo, Nsenkwa, Mtakuja, Wachawaseme, Utende, Ilunde na Isegenezya na tayari visima vyote ishirini na moja vinatumika kama ilivyokusudiwa.

Mifumo ya uvunaji maji ya mvua

Halmashauri pia itatekeleza ujenzi wa miradi ya uvunaji maji ya mvua katika baadhi ya maeneo ili kuondoa tatizo la maji kwa wananchi. Mfano wa miradi hiyo ni miradi ya uvunaji maji ya mvua Inyonga, Ilunde na Wachawaseme. Pia wananchi wamekuwa wakihamasishwa kutekeleza mifumo ya uvunaji wa maji ya mvua katika kukabiliana na tatizo la maji kwa wananchi wetu.

Maji ya kutega

Pia katika kuhakikisha huduma ya maji inapatikana kwa uhakika kwa wananchi Halmashauri ipo katika hatua ya usanifu wa ujenzi wa Mabwawa mawili katika Kata ya Nsenkwa na Ilunde, maamuzi ya usanifu yaliamuliwa na timu maalumu iliyotumwa na Wizara ya Maji na Umwagiliaji kubaini maeneo yenye sifa  za kujengwa Bwawa, Timu hii ilifanya utafiti na kubaini maeneo tajwa hapo juu yanasifa.

 

MALENGO YA IDARA YA MAJI:

  1. Kuhakikisha upatikanaji wa maji kwa wananchi katika umbali wa kutembea (kwa miguu) usiozidi mita 400 kutoka 42.1% ya sasa hadi 80% ifikapo Juni 2017 kwa kutekeleza yafuatayo.
    1. Usimamizi na ufuatiliaji wa miradi ya maji iliyokamilika ambapo huduma ya maji inapatikana kwa uhakika.
    2. Usimamizi na ufuatiliaji wa miradi ya maji inayotekelezwa chini ya mpango wa maendeleo ya sekta ya maji kwa ufadhili wa wahisani na Serikali ya Jamhuri ya Tanzania
    3. Ukarabati wa miradi ya maji.
    4. Ujenzi miradi mipya ya maji.
    5. Upanuzi wa miradi ya maji ili kufikisha huduma katika maeneo ya jirani ilipo miradi inayotoa huduma.
  2. Kutoa elimu ya uundwaji wa Jumuiya za watumiaji maji pamoja na kuunda jumuiya husika.
  3. Kutoa Elimu ya usafi wa mazingira na usafi wa unawaji mikono kabla ya kula, unawaji mikono kwa maji na sabuni baada ya kutoka chooni, ujenzi wa vyoo bora na matumizi bora  kuepuka magonjwa ya mlipuko.
  1. Kutoa elimu ya uhifadhi wa mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji pamoja na upandaji wa miti rafiki ya maji kuzunguka au karibu na maeneo ya vyanzo vya maji.

HALI YA UTEKELEZAJI WA MALENGO YA IDARA 

Halmashauri kupitia Idara ya Maji katika kuhakikisha inatimiza wajibu wake wa kupeleka huduma ya maji kwa wananchi na kutekeleza malengo ya kiidara imesimamia na kutekeleza yafuatayo:-

  1. Kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi.

Usimamizi na ufuatiliaji wa miradi ya maji iliyokamilika ambapo huduma ya maji inapatikana kwa uhakika.

NA.

KIJIJI

 

AINA YA MRADI

MAELEZO

 

 

 

mmmmm/MMMMMMMMmmm

1.
Mapili
Uchimbaji wa visima viwili virefu
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa.
2.
Ipwaga
Uchimbaji wa kisima kirefu
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa.
3
Mtakuja
Uchimbaji wa kisima kirefu
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa.
4.
Kaulolo
Uchimbaji wa kisima kirefu
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa.
5
Nsenkwa
Uchimbaji wa kisima kirefu
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa.
6
Wachawaseme
Uchimbaji wa kisima kirefu
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa..
7
Utende
Uchimbaji wa kisima kirefu
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa.
8
Inyonga
Uchimbaji wa kisima kirefu
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa.
9
Kamalampaka
Uchimbaji wa visima viwili virefu.
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa.
10
Kalovya
Uchimbaji wa visima viwili virefu
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa.
11
Kamsisi
Uchimbaji wa visima viwili virefu
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa..
12
Songambele
Uchimbaji wa kisima kirefu
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa.
13
Imalauduki
Uchimbaji wa kisima kirefu
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa.
14
Nsenkwa
Uchimbaji wa kisima kirefu
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa..
15
Ilunde
Uchimbaji wa kisima kirefu
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa.
16
Isegenezya
Uchimbaji wa Visima viwili virefu
Kazi ya uchimbaji imekamilika na wananchi wanapata huduma ya maji kama ilivyokusudiwa.

 

Usimamizi na ufuatiliaji wa miradi ya maji inayotekelezwa chini ya mpango wa maendeleo ya sekta ya maji kwa ufadhili wa wahisani na Serikali ya Jamhuri ya Tanzania

 

 

 

 

NA
KIJIJI
 
AINA YA MRADI ILIYOTEKELEZWA 
HATUA YA UTEKELEZAJI
MAELEZO 
1.
Mamba
Mradi wa maji ya bomba katika kijiji cha Mamba unaofadhiliwa na Benki ya Dunia na Serikali ya Tanzania.
Utekelezaji wa mradi huu umekamilika na mradi unatumika pia mradi upo hatua ya matazamio.
Utekelezaji wa mradi huu umekamilika na mradi unatumika pia mradi upo hatua ya matazamio.

 

 

Ujenzi wa miradi mipya

NA
KIJIJI
 
AINA YA MRADI 
HATUA YA UTEKELEZAJI
 
 
 
mmmmm/MMMMMMMMmmm
GHARAMA/MAELEZO  
1
Mapili
Mradi wa maji ya bomba katika kijiji cha Mapili unaofadhiliwa na Serikali ya Tanzania.
Utekelezaji wa mradi huu upo hatua ya Zabuni.
Utekelezaji wa mradi huu upo hatua ya zabuni.
2
Nsenkwa
Mradi wa maji ya bomba katika kijiji cha Nsenkwa unaofadhiliwa na Serikali ya Tanzania.
Utekelezaji wa mradi huu upo hatua ya Zabuni.
Utekelezaji wa mradi huu upo hatua ya zabuni.
3
Inyonga
Mradi wa maji ya bomba katika kijiji cha Inyonga unaofadhiliwa na Serikali ya Tanzania.
Utekelezaji wa mradi huu upo hatua ya Zabuni.
Utekelezaji wa mradi huu upo hatua ya zabuni.
4
Wachawaseme
Mradi wa maji ya bomba katika kijiji cha Wachawaseme unaofadhiliwa na Serikali ya Tanzania.
Utekelezaji wa mradi huu upo hatua ya Zabuni.
Utekelezaji wa mradi huu upo hatua ya zabuni.
5
Ilunde
Mradi wa maji ya bomba katika kijiji cha Ilunde unaofadhiliwa na Serikali ya Tanzania.
Utekelezaji wa mradi huu upo hatua ya Zabuni.
Utekelezaji wa mradi huu upo hatua ya zabuni.
6
Kamsisi
Mradi wa maji ya bomba katika kijiji cha Kamsisi unaofadhiliwa na Serikali ya Tanzania.
Utekelezaji wa mradi huu upo hatua ya Zabuni.
Utekelezaji wa mradi huu upo hatua ya zabuni.

Kutoa elimu ya usafi wa mazingira na uundwaji wa jumuiya za watumiaji maji.

Katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2016/2017 palikuwa na zoezi la utoaji wa mafunzo kwa jumuiya za watumiaji maji na usajili wa jumuiya za watumiaji maji.

Elimu ya usafi wa mazingira na unawaji mikono kabla ya kula, unawaji mikono kwa maji na sabuni baada ya kutoka chooni elimu hii huletwa kupitia programu ya SWASH na programu ya usambazaji maji vijijini (RWSSP) chini ya kipengele cha usafi wa mazingira. Utekelezaji wa elimu hii utasaidia kupunguza magonjwa ya mlipuko kwa wananchi hasa watoto.  Hakukuwa na utoaji wa huduma hii kutokana na tatizo la ukosefu wa fedha.

Uhifadhi wa mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji

Elimu ya utunzaji / uhifadhi wa mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji ilitolewa wakati wa zoezi la usajili wa jumuiya za watumiaji maji (COWSOs) kutokana na ukosefu wa fedha za utekelezaji.

 

CHANGAMOTO:

Halmashauri kupitia idara ya maji inakabiliwa na changamoto zifuatazo katika utekelezaji wa majukumu yake:-

 

  1. Wananchi kutokuwa tayari kuchangia huduma ya maji kwa uendelevu wa miradi husika kwa baadhi ya vijiji.
  2. Upungufu wa watumishi.
  1. Ukosefu wa usafiri kwa wataalamu katika kusimamia shughuli zinazohusu idara ya maji mfano usimamizi wa ujenzi, ukarabati wa miundo mbinu, utoaji elimu juu ya utunzaji wa miundo mbinu ya maji na usajili wa jumuiya za watumiaji maji (COWSO) pamoja na vyanzo vya maji na ukusanyaji wa taarifa sahihi zihusuzo upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi.

UTATUZI WA CHANGAMOTO

  1. Halmashuri inaendelea kutoa hamasa kwa wanachi wachangie huduma ya maji kwa manufaa ya sasa na ya baadae.
  2. Halmashauri imeomba kuongezewa watumishi katika mamlaka zinazohusika na watumishi.
  3. Katika kutatua tatizo la usafiri Halmashauri inaendela kuwa na matumizi shirikishi kwa idara mbalimbali kwa magari machache yaliyopo katika Halmashauri, ambapo Halmashauri ina magari machache ambayo hayakidhi mahitaji ya kila Idara. Lakini pia Halmashauri imewasilisha ombi Wizara ya maji na umwagiliaji la kupatiwa usafiri kwa watumishi wa idara ya maji ili waweze kutimiza malengo ya kuhakikisha wananchi wa Jimbo la Katavi wanapata huduma ya maji safi na salama kwa umbali usiozidi mita 400.

Naomba kuwasilisha

Matangazo

  • MAPOKEZI YA MWENGE April 09, 2017
  • WIMBO WA MWENGE April 09, 2017
  • TANGAZO LA KUNYWA DAWA ZA MINYOO YA TUMBO April 26, 2017
  • Nafasi za kazi mbalimbali serikalini July 11, 2018
  • Waonaji wote

Habari Mpya

  • Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uwekezaji) Prof. Kitila Mkumbo

    March 05, 2021
  • Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homera

    March 05, 2021
  • ziara ya Mkuu wa Mkoa kukagua miradi ya maendeleo.

    February 24, 2021
  • Mkuu wa Mkoa Katavi Mhe, Juma Homera na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Wilaya Mlele

    February 24, 2021
  • Waonaji wote

Video

KATUNI SAFI KWA AJILI YA WATOTO
Video Zaidi

wavuti za Haraka

  • FACE BOOK PAGE YA MLELE
  • MLELE DC BLOG
  • kilimo na umwagiliaji
  • mafunzo tovuti za serikali kanda ya magharibi
  • MAONESHO

Wavuti Mwambata

  • Wizara ya Utumishi wa Umma
  • Tume ya ajira ya Tanzania
  • Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania
  • Jamhuri ya muungano wa tanzania
  • Tawala za mikoa na Serikali za mitaa
  • BARAZA LA MITIHANI

Takwimu za Watembeleaji

world map hits counter

Hesabu Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mlele

    Anuani ya Posta: S.L.P 686 MPANDA

    Simu: +255759023788

    Simu ya Kiganjani: 0759023788

    Barua pepe: ded@mleledc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ya @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Mlele. Hakizote zimehifadhiwa