• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watuishi |
Mlele District Council
Mlele District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Maji
        • Historia
        • Dhima na Dira
        • Muundo wa Taasisi
        • Ukaribisho
        • Jaribu
        • what we do
        • Huduma ya Maji
        • Huduma za Afya
        • Elimu Msingi
        • Huduma
        • Mwenyekiti wa Halmashauri
        • Mkurugenzi Mtendaji
        • Utawala na Rasilimali watu
        • /TEHAMA-na-Takwimu
        • Idara ya Afya na Ustawi wa Jamii
        • Mipango takwimu na Ufuatiaji
        • Ardhi na Maliasili
        • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Sheria
        • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maendeleo ya Jamii
        • Idara
        • Vitengo
        • Ujenzi
        • Maji
        • Ugavi na Manunuzi
        • Usafishaji na Mazingira
        • Uchaguzi
        • Tasaf III
        • Mainstreaming Sustainable Forest Managment in Woodland of Western Tanzania Project
        • Mwenge waUhuru
        • UKIMWI/ VVU
        • Risk Oficer Cordinator
        • Miradi inayoendelea
        • Zabuni
        • Kazi za Idara Utumishi
        • Muundo wa Halmashauri
        • Miradi Lengwa
        • Kitengo cha nyuki
        • Mwenge
        • Sera ya Faragha
        • Kanusho
        • Machapisho
        • Sheria
        • MTF
        • Fomu
        • Orodha ya Madiwani
        • Fedha, Uongozi na Mipango
        • UKIMWI
        • Maji
        • Mipango Miji na Mazingira
        • Uchumi, Afya na Elimu
        • Maadili
        • Ratiba
        • Vikao vya waheshimiwa
        • Kuonana na Mwenyekiti
        • Madiwani
        • Kanausho
        • Huduma ya Maji
        • Huduma ya Afya
        • Huduma ya Kilimo
        • Huduma ya Elimu
        • Huduma ya Ufugaji
        • Huduma za Uvuvi
        • Huduma za Sheria
        • Huduma za kiutumishi
        • Vivutio vya Utalii
        • Kilimo
        • Ufugaji
        • Itakayo tekelezwa
        • Inayoendelea
        • Iliyo Tekelezwa
        • muongozo
        • Sheria Ndogo
        • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
        • Mpango Mkakati
        • Taarifa
        • Fomu Mbalimbali
        • Taarifa kwa Umma
        • Video za shughuli zetu
        • Maktaba ya Picha
        • Magazeti
        • Hotuba
        • ORODHA YA WAJUMBE WA KAMATI MBALIMBALI ZA KUDUMUKWA MWAKA WA FEDHA 2019/2020
        • KARENDA YA VIKAO VYA KISHERIA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA MLELE KWA MWAKA WA FEDHA 2019/2020
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya
    • Viengo
      • Kitengo cha TEHAMA na Mahusiano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Uchaguzi Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Kilimo na Umwagiliaji
    • Huduma za Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orotha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Mazingira
      • UKIMWI
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa
      • Kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayotekelezwa
    • Iliyotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kiini cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Album ya Picha
    • Video
    • Hotuba
  • TASAF

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURU WA MUUNGANO WA TANZANIA

Posted on: April 4th, 2019


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 04 Aprili, 2019 amemaliza ziara yake ya siku 3 Mkoani Mtwara kwa kufungua Kituo cha Afya cha Mbonde kilichopo katika Wilaya ya Masasi na kufungua barabara za Mangaka – Nakapanya – Tunduru na Mangaka - Mtambaswala.

Kituo cha Afya cha Mbonde kilichojengwa kwa gharama ya shilingi Milioni 500 ni miongoni mwa Vituo vya Afya vipya 13 vilivyojengwa Mkoani Mtwara na ni miongoni mwa Vituo vya Afya vipya 352 vilivyojengwa nchi nzima katika kipindi cha miezi 18 iliyopita vikiwa na uwezo wa kutoa huduma za matibabu mbalimbali ikiwemo matibabu ya upasuaji.

Akiwa kituoni hapo, Mhe. Rais Magufuli amejionea miundombinu yake ikiwemo wodi za kulala wagonjwa, maabara, vyumba vya upasuaji vyenye vifaa vya kisasa na majengo mapya.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kuendelea kutilia mkazo uwekezaji katika miundombinu ya kutolea huduma za afya pamoja na kutoa maelekezo yenye manufaa ikiwemo kuagiza ununuzi wa vifaa ufanyike moja kwa moja kutoka kwa watengenezaji moja kwa moja, hali iliyosaidia kuokoa gharama za ununuzi zikiwemo mashine za usingizi ambazo zimenunuliwa kwa shilingi Milioni 50 badala ya shilingi Milioni 100 kwa kila mashine moja.

Nae Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo amesema Serikali ya Awamu ya Tano imefanikiwa kujenga Vituo vya Afya 352 na hospitali 67 nchi nzima katika kipindi cha miezi 18 ikilinganishwa na hospitali 77 zilizokuwa zimejengwa tangu Uhuru, na kwamba katika bajeti ijayo vituo vya afya vingine 27 vitajengwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Akizungumza baada ya kufungua Kituo cha Afya cha Mbonde Mhe. Rais Magufuli amewapongeza wananchi wa Masasi kwa kupata kituo hicho na ameeleza kuwa Serikali imetumia shilingi Bilioni 184 kujenga vituo vyote 352 nchi nzima kwa lengo la kuhakikisha Watanzania wanapata huduma za uhakika za matibabu jirani na maeneo wanayoishi.

Mhe. Rais Magufuli ameipongeza Wizara ya Afya na TAMISEMI kwa kuhakikisha ujenzi wa vituo vya afya unafanyika vizuri na amebainisha kuwa pamoja na kujenga miundombinu hiyo pia imejenga nyumba 306 za watumishi wa afya, imeajiri madaktari 11,200 na kuimarisha huduma za matibabu ya kibingwa katika hosptali ya Taifa Muhimbili na hospitali nyingine za rufaa hali iliyowezesha nchi jirani kuitegemea Tanzania kwa matibabu.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amekubali ombi la Mbunge wa Lulindi Mhe. Jerome Bwanausi la kujengwa kwa kilometa 40 za barabara ya lami kati ya Mpeta na Newala na pia ameahidi kutoa gari la wagonjwa kwa ajili ya kituo cha afya cha Mbonde baada ya gari lililokuwepo kuchomwa moto wakati wa vurugu.

Mhe. Rais Magufuli ameiagiza Wizara ya Kilimo na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kuhakikisha viwanda vyote vya korosho vilivyobinafsishwa lakini havifanyi kazi vinanyang’anywa haraka na amemtaka Naibu Katibu Mkuu wa Viwanda Bw. Ludovick Nduhiye kutoondoka Mtwara mpaka ahakikishe agizo hilo limetekelezwa.

Kabla ya kuondoka Masasi kuelekea Nanyumbu Mhe. Rais Magufuli ametembelea Ofisi ya Chama Cha Mapinduzi ya Wilaya ya Masasi ambayo ilikumbwa na kadhia ya kuchomwa moto na waandamanaji mwaka 2013 ambapo amechangia shilingi Milioni 20 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa ofisi mpya, amechangia shilingi Milioni 5 kwa Shule ya Msingi Mkuti na ametoa wito kwa wananchi wa Masasi kujiepusha na mihemko ya hasira inayosababisha uharibifu wa mali.

Mhe. Rais Magufuli pia amechangia shilingi Milioni 5 kwa shule ya Sekondari Mikangaula kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya shule hiyo na ameagiza shule hiyo iwekewe umeme ndani ya miezi 2.

“Nitawapa shilingi Milioni 5 zikawasaidie kujenga miundombinu ya shule, na umeme mtapata, lakini nitoe wito kwenu na kwa wanafunzi wote Tanzania kusoma kwa juhudi kwa sababu sasa hivi elimu inatolewa bila malipo na mkifika vyuo vikuu mtapata mikopo” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Akiwa Mangaka Wilayani Nanyumbu Mhe. Rais Magufuli amefungua barabara ya lami ya Mangaka – Nakapanya – Tunduru yenye urefu wa kilometa 137 na ambayo imejengwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 126.3 na barabara ya lami ya Mangaka – Mtambaswala yenye urefu wa kilometa 65.5 na imejengwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 56.2.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe amesema kukamilika kwa barabara hizo pamoja na miradi mingine ya barabara kuu kumefikisha jumla ya kilometa 957 (kupitia Mingoyo) na hivyo kukamilisha mpango wa ujenzi wa barabara za lami za ushoroba wa kusini unaounganisha Mbambabay mpaka Mtwara.

Barabara hizo zimejengwa kwa ushirikiano wa Serikali ya Tanzania na Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA).

Akizungumza na wananchi wa Nanyumbu katika sherehe za ufunguzi wa barabara hizo Mhe. Rais Magufuli amewashukuru Marais Wastaafu Mhe. Benjamin William Mkapa na Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kukubali mawazo yake ya kujengwa barabara hizo akiwa Waziri wa Ujenzi na pia ameishukuru AfDB na JICA kwa ufadhili mkubwa walioutoa kufanikisha ujenzi wa barabara hizo.

Mhe. Rais Magufuli amewapongeza wananchi wa Mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma kwa kufanikiwa kupata barabara hizo na hivyo kuondokana na adha ya hali mbaya ya barabara iliyowasumbua kwa miaka mingi na kusababisha shughuli nyingi za kiuchumi kudorola.

Kuhusu ujenzi wa barabara ya Mnivata – Tandahimba – Newala – Masasi, Mhe. Rais Magufuli ameiagiza Wizara ya Fedha na Mipango na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kuwasilisha andika la kuomba ufadhili wa ujenzi wa barabara hiyo Jumatatu ijayo (08 Aprili, 2019) baada ya Balozi wa Japan hapa nchini Mhe. Shinichi Goto na Mwakilishi wa JICA Bw. Yasunori Onishi ambao wamehudhuria sherehe hiyo kuonesha utayari wa kutoa fedha.

Mhe. Rais Magufuli ametoa siku 5 kwa Baraza la Taifa la Menejimenti ya Mazingira (NEMC) kutoa vibali kwa mwekezaji anayesubiri kibali ili aweze kusafirisha tani Milioni 1 za makaa ya mawe kwenda nje ya nchi kupitia bandari ya Mtwara

Katika salamu zake za kumuaga Mhe. Rais Magufuli Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa ziara yake Mkoani Mtwara na ameahidi kuwa maelekezo yote aliyoyatoa yatatekelezwa.

Mhe. Rais Magufuli amewashukuru wananchi wa Mtwara kwa mapokezi na kujitokeza kwa wingi katika mikutano na katika miradi aliyoiweka mawe ya msingi na kuifungua na ameongeza kuwa “najua baadhi yenu mlijitokeza kutaka tusalimiane kandokando ya barabara lakini sikufanikiwa kwa kuwa nisingeweza kukutana nanyi usiku, lakini tambueni kuwa tupo pamoja na nawapenda sana”.

 

 

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Nanyumbu

04 Aprili, 2019

Matangazo

  • TANGAZO KUTOKA TUME HURU YA UCHAGUZI March 03, 2025
  • MABADILIKO YA UKUMBI WA USAILI MLELE DC October 04, 2024
  • Tangazo la Ajira ya ukusanyaji wa Mapato July 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI MBALIMBALI ZA AFYA December 10, 2021
  • Waonaji wote

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA PEPMIS KWA WATAALAMU

    June 03, 2025
  • MUONEKANO ANGAVU WA HOSPITALI YA WILAYA YA MLELE

    May 26, 2025
  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI DODOM

    May 23, 2025
  • MAENDELEO YA UJENZI WA SHULE SHIKIZI

    April 03, 2025
  • Waonaji wote

Video

#TBC LIVE ZOOM: YALIYOJIRI NA MAFANIKIO YA ZIARA YA RAIS SAMIA NCHINI QATAR
Video Zaidi

wavuti za Haraka

  • FACE BOOK PAGE YA MLELE
  • MLELE DC BLOG
  • kilimo na umwagiliaji
  • mafunzo tovuti za serikali kanda ya magharibi
  • MAONESHO
  • Tuma barua pepe hapa

Wavuti Mwambata

  • Wizara ya Utumishi wa Umma
  • Tume ya ajira ya Tanzania
  • Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania
  • Jamhuri ya muungano wa tanzania
  • Tawala za mikoa na Serikali za mitaa
  • BARAZA LA MITIHANI

Takwimu za Watembeleaji

world map hits counter

Hesabu Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mlele

    Anuani ya Posta: S.L.P 686 MPANDA

    Simu: +25525295197

    Simu ya Kiganjani: 0786077372

    Barua pepe: ded@mleledc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ya @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Mlele. Hakizote zimehifadhiwa